Kufuatia tetemeko lililotokea mkoani Kagera September 10
mwaka jana na kusababisha athari kubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo
zahanati ya Kabyaile iliyopo kata Ishozi wilayani Misenyi,baadhi ya wananchi
wameeleza changamoto walizokumbana nazo mpaka sasa.
Mkazi mmoja wa eneo hilo Bi,Restuta Isaya amesema kuwa kwa upande wake imemuathiri kwa kiwango kikubwa maana baada ya kutokea tetemeko walitengewa maeneo ya kupata huduma kwa muda wakati jitihada za kurudisha miundombinu zinaendelea.
Aidha amesema kuwa alifika katika eneo hilo wakati anaenda
kujifungua lakini walimfukuza na kumwambia aende katika hospital teule ya
wilaya Mgana na kuongeza kuwa mtoto alikuwa anakaribia,kitendo kilichopelekea
kukodi pikipiki kwa zaidi ya elfu 20 ili awahi huduma Mgana Hospital.
Sanjali na hayo ameipongeza serikali kwa kukamilisha kituo
cha afya Kabyaile na kukikabidhi kwa halmashauri,ambapo amewaomba wahudumu
watakaofanya kazi katika kituo hicho kuwajali wananchi ili wapate huduma
stahiki.
……….…………………………………….TAZAMA VIDEO HAPA……………………………………………
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment