MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 22 July 2017

WAZIRI MWIGULU ALIVYOFUNGUA GEREZA LA KITENGULE


Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba leo amefungua gereza la kilimo la Kitengule lilopo wilayani Karagwe mkoani Kagera lililogharimu zaidi ya million 100 ambalo ni miongoni mwa majengo yaliyoathirika kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo September 10 mwaka jana.

Baada ya ufunguzi  huo waziri Mwigulu amesema kuwa  ndani ya siku tatu waanze mpango wa kurudisha wafungwa waliokuwa wamehamishiwa gereza jirani la Mwisa ili kupunguza msongamano uliopo ndani ya gereza hilo.

Aidha wakazi wa maeneo hayo wamesema kuwa kuna changamoto ya wanyama wakali kuingia karibu na makazi yao hali inayowapa hofu kutokana na eneo hilo kuwa asili ya pori,ambapo waziri Mwigulu amesema kuwa changamoto hiyo ameichukua na ataifanyia kazi.

PICHA KATIKA UFUNGUZI HUO..........................................................................


Na Mwanaharakati.

No comments: