MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 21 July 2017

KAULI YA IGP SIRRO KUHUSU KINACHOENDELEA KIBITI

 


Baada ya ziara ya Rais Magufuli mkoani Kagera,baadhi ya viongozi nchini Tanzania,leo Mkuu wa jeshi la polisi Tanzania IGP Simon Sirro amefanya ziara yake mkoani humo ambapo amekutana na askari wa mkoa Kagera.

Baada ya mazungumzo na askari hao,IGP Sirro amesema kuwa miongoni mwa vitu alivyoongea nao ni pamoja na hali inayoendelea Kibiti juu ya mauaji ya wananchi na kusema kuwa sasa hivi hali inaendelea vizuri maana wameanza kuwaondoa majambazi ikiwa ni pamoja na kuwaua huku akiutaka mkoa wa Kagera kutoa ushirikiano ili kukomesha vitendo hivyo.

Ameongeza kuwa watu hao wanaweza hata kuamia mkoani Kagera na kusababisha madhara makubwa huku akiwataka wanakagera wote kutoa ushirikiano pale wanapokuwa na mashaka kwa mtu mgeni ili kama atakuwa miongoni mwa majambazi hao aweze kuchukuliwa hatua.



Na Mwanaharakati.

No comments: