MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 6 March 2012

 Hapa juu hii ndiyo meza na Chemri vilivyoko kwenye chumba kinacholipiwa shilingi za kitanzania elfu nane(8,000) kwa usiku mmoja, na hii ni Gest ambayo jina lake limehifadhiwa.
 Hivi ni viatu aina ya Yeboyebo anavyopewa mteja kwa matumizi kama kanda mbili.Chini ni Bafu la kuogea lakini rangi zinazoonekana ni uchafu ambao unateleza na kuna harufu mbaya unapooga, bahati mbaya sabuni haikuwepo wala tauro hivyo ni juhudi za mteja mwenyewe
 Nilipofanya mahojiano na mama huyu amabAye pia hakupenda niweke jina lake kwenye vyombo, japo nilichukuwa picha hii kupitia mashine maalum, anasema gest hiyo ina jumla ya vyumba 18 na Bosi mwenyewe wala hana mpango wa kurekebisha chochote kwani wateja wanalipa, na nilipohoji aina ya wateja alisema hasa ni wasafiri ambao wanashuka kwenye mabasi kwani hawana pa kwenda vyumba vikiisha kwenye gest zingine.
JE! WADAU TUFANYE NINI KATIKA HILI AU TUYAFUMBIE MACHO TUENDELEE KUUMIA?

No comments: