MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 9 March 2012

 Juu ni sura ya mbele ya shule hiyo iliyopo kata Katoke wilayani Muleba, na chini ni sehemu moja wapo ya jengo la shule hiyo yenye madarasa kadhaa na inatarajiwa kupokea wanafunzi wa Bweni wasichana.
 Akizungumzia mgogoro unaosemekana kuwepo kati ya wananchi na mbunge huyo Ruth Msafiri, amesema yeye anavyojua hakuna mgogoro kwasababu eneo hilo alipewa na serikali ya kijiji kupitia VDC miaka kumi iliyopita hivyo marumbano hayo yanapikwa kisiasa.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na Kamera hii wamesema eneo lenye ukubwa wa ekari 40 alipewa baada ya kuliomba kuwa anajenga shule ya kijamii lakini baada ya kushindwa ubunge ameamua kujitwalia kuwa anajenga shule binafsi, na wengine wanasema ni shule yake kwasababu hakuna mchango wowote wa mwananchi.

Mapema mwezi februari, mkuu wa mkoa wa Kagera alifanya ziara katika kata hiyo na alipopewa taarifa aliwataka viongozi wa VDC na WDC kukaa pamoja kupata ufumbuzi lakini akazuia wasijenge shule nyingine kabla ya kukamilisha walizokwishaanzisha.

Mpaka sasa hali ni tete kutokana kuwa kuwepo vikao mbalimbali vya baadhi ya viongozi WDC ikilaumu lakini yeye Ruth akisema VDC ilimpa kihalali.

No comments: