MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 10 March 2012

Hapa juu hili ni jengo la chama cha ushirika ambalo liko jirani na shule ya msingi Katoke "B" ambayo iliezuliwa na upepo vyumba viwili vya madarasa ziliponyesha mvua tarehe 22 Feb 2012.Chini wanafunzi 90 wa darasa la kwanza wakisoma katika kijengo hicho kidogo na taarifa zinzsema kuna hewa nzito kwani hakina madirisha na kuna giza. 
Chini ni sehemu ya jengo la shule lililobomoka ambalo hata hivyo limechakaa baada ya kukaa muda mrefu bila ukarabati tangu ilipoanzishwa mwaka 1935.
 Pamoja na madarasa mawili yaliyosalia, bado ni taabu kwao kuyatumia kwani shule ina wanafunzi 480 ambapo wa awali ni 50 na 430.
Huyu chini ni mtendaji wa Kata ya Katoke FAUSTNE RWEYEMAMU, kwa upande wake amesema tatizo hilo linafanyiwa ufumbuzi baada ya kuhamasisha wananchi kuchangia nguvu kazi sambamba na michango ya fedha zitakazo pitishwa baada ya kamati ya kata itakayokaa leo jumamosi kujadili hali hiyo.
Ufaulu wa wanafunzi mwaka 2011 darasa la saba, kati ya wanafunzi 69 wameshinda 49 kujiunga kidato cha kwanza, ambapo kwa mujibu wa mratibu elimu kata hiyo Bwana JULIUS KATALE jumla au zaidi ya wanafunzi 200 wa kata nzima walichaguliwa kwenda kidato cha kwanza ila kutokana na mgogoro wa kata kutokuwa na shule ya kata walikuwa wamesalia wanafunzi 96, ambao hata hivyo wamekubaliwa kuendele kusoma katika shule ya kata Izigo.

Kata hiyo inakabiliwa na mgogoro wa kutokuwa na shule ya kutokana na kutegemea iliyojengwa na mbunge wa zamani RUTH MSAFIRI ambayo ni shule yake binafsi lakini hata hivyo bado haijamilika ujenzi wake.

No comments: