MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 15 April 2012

MVUA MANISPAA YA BUKOBA ZAASHIRIA MAFURIKO KUTOKANA NA UJENZI HOLELA;-

 
 Picha juu ni eneo linalotumika kufanyia biashara ndogondogo lakini asubuhi ya leo maji yamejaa kiasi kwamba hakuna kinachoweza kufanyika hadi maji yapungue, CHINI ni majengo yaliyojengwa ndani ya mto Kanoni nyuma ya Hotel ya PRINCE MOTEL ambapo inaonekana hapo ndipo maji yanakwama kwa kiasi kikubwa.

 CHINI ni picha iliyochukuliwa wakti wa mvua asubuhi leo katika moja ya daraja la Brabara ya Kashozi eneo la machinjioni katika manipaa ya Bukoba.
 Katika eneo la makaazi ya watu kumekuwa na uwingi wa maji unaotokana na miundombinu mibovu inayoharibiwa na wananchi kwa kuje holela, hata kama serikali ya mkoa inajitahidi kuboresha miundombinu hiyo.
Awali mkuu wa mkoa wa Kagera kanali mstaafu FABIAEN MASSAWE aliwataka viongozi wa miundombinu kwa kushirikiana na afisa afya kuhakikisha wanasafisha mitaro ukiwemo mto mkubwa katika manispaa hiyo.
CHINI ni mtaro mmojawapo wa maji ambao unalemewa kupitisha maji kipindi cha mvua kutokana na udogo wake.

No comments: