MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 6 April 2012

RAIS ATOA ZAWADI ZA PASAKA KWA WAZEE BUKOBA;

Rais wa jamhuri ya Muungano Tanzania JAKAYA MRISHO KIKWTE,ametoa  zawadi za sikukuu ya pasaka kwa wazee wanaolelewa katika kituo cha wazee Kilima Bukoiba vijijinji.



Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Rais Kanali MASSAWE amekabidhi zawadi hizo kwa niaba ya rais wa Jamhuri ya ya muungano Mh JAKAYA MRISHO KIKWETE.
Rais KIKWETE ametoa kilo miamoja za mchele, lita 40 za mafuta ya kula na mbuzi wawili kwa wazee hao kwa ajili ya kuwafariji katika kusherehekea sikukuu ya Pasaka.
Amesema kuwa yuko nao bega kwa bega katika kuhakikisha wanayamudu maisha waliyonayo, kwa kuwataka wasjione wapweke katika kipindi hiki cha sikukuu pamoja kuahdi kuendelea kufuatilia maisha yao katika kituo hicho cha kilima chenye wazee 15 wakiwemo wanaume 9 na wanawake 6, pamoja na watoto yatima 13 wasiyojiweza.


 Kanali MASSAWE amewataka viongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kuwa na shamba la kituo ambalo litasaidia wazee hao baadhi wenye nguvu kujishughulisha ili kuweka afya zao katika hali nzuri ya kuchangamka.

Mkuu huyo wa mkoa, amekabidhi shilingi elfu 20 kwa mkuu wa kituo hicho Bi CREMENTINA MARTINE kwa kuanzia kununulia majembe matano, ambapo amemtaka mkuu huyo wa kituo kushirikiana na mtendaji wa eneo hilo kuandaa utaratibu wa kuanzisha shmaba kwa kualika wadau mbalimbali ili washiriki kuanzisha shamba hilo.

 Kito hicho kina jumla ya wtoto 12 ambapo wanne wanasoma shule ya sekondari Kabugaro na wengine 8 wako katika madarasa ya kwanza na la saba.
Ni mmoja wa wazee hao akiwa chumbani kwake kituoni hapo.

No comments: