MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 7 May 2012

UTAFITI MARUKUKUPITIA KANDA YA ZIWA UMEZINDUA MRADI WA VIAZI RISHE;-

Pichani chini ni miongoni mwa viazi rishe vinavyoelekezwa kulimwa katika mashamba ya wakulima kwa wingi kwani hata hivyo vina tibu magonjwa sugu kama saratani na kansa.
Akizungumza na wadau wa kilimo na biashara mkoani humo, mtafiti wa mazao ya kilimo Bwana INNOCENT NDYETABULA, amesema kuwa wananchi wakijikita kufanya kilimo cha viazi rishe kwa kufauata maelekezo ya wataalamu watajipatia chakula cha kutosha na kukuza uchumi.
Bwa Ndyetabula amesema hayo kwenye mkutano wa uzinduzi wa mradi wa viazi rishe utakaoendeshwa kwenye wilaya za Muleba na Misenyi mkoani Kagera.
Naye mtaalamu wa vimelea vya magonjwa ya mimea Dokta MAGDALENA WILLIUM, amewata wananchi kutobagua vyakula vya asili hasa viazi rishe, kwani pamoja na kuongeza uchumi kwa wananchi, pia vinatibu magonjwa sugu mbalimbali.
Mradi wa kanda ya ziwa wa agricultural imformation system on  orange sweet potatoe , umezinduliwa na taasisi ya utafiti wa kilimo MARUKU, na utafanya kazi katika wailaya mbili za MULEBA na MISENYI mkoani  Kagera  kwa kushirikisha makundi ya wakulima katika wilaya hizo, na umeanza mwezi Machi mwaka huu.

No comments: