MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 29 August 2012

MAANDALIZI YA MKUTANO WA 11 WA HALMASHAURI 130 NCHI ZA UGANDA, KENYA NA TANZANIA-LVRLAC

Mwenyekiti wa Umoja huo hapa nchini, Dk ANATOLI  AMANI amesema kuwa Mkutano huo wa LVRLAC,  utaenda sambamba na viongozi hao kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya manispaa ya Bukoba.

Hatua hiyo  ni kuunga mkono jitihada za Mkuu wa mkoa wa KAGERA, kanali mstaafu FABIAN MASAWE.
Wakurugenzi wa Halmashauri, Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri 28 za Tanzania ambao wanahudhuria  mkutano huo,  jana, walishiriki katika semina ya kuwajengea uwezo namna ya kubuni miradi ya maendeleo katika Halmashauri zao ili kuongeza mapato.

Katika semina hiyo,  baadhi ya Halmashauri zimependekeza miradi kadhaa ya maendeleo ambayo zitaitafutia wafadhili. 

Halmashauri  za mkoa wa KAGERA  kwa pamoja zimependekeza ujenzi wa maegesho mapya ya magari, ujenzi wa viwanja bora vya michezo,  pamoja na kuimarisha msitu wa BURIGI,  kuwa moja ya kivutio cha utalii mkoani KAGERA.

Akifunga semina hiyo ya siku moja, Mkuu wa wilaya ya BUKOBA, bi ZIPORRAH PANGANI  amewataka viongozi hao kujenga desturi ya kuwashirikisha wananchi katika kupanga na wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
 Hapa juu ni ukumbi wa utakaotumika kufanya mkutano huo ambao hadi sasa uko kwenye maandalizi
 Kama ilivyo ada kunapokuwa upokeaji wa geni lazima usafi uzingatiwe, hii ni shimo la taka ambalo linakaa na uchafu muda mrefu lakini sasa naona itifaki imezingatiwa.

No comments: