MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 30 August 2012

MKUTANO WA 11 WA HLMASHAURI 130 ZA EAC LVRLAC

Mkuu wa mkoa wa KAGERA, kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, leo ameufungua rasmi Mkutano wa 11 wa Umoja wa  Halmashauri 130 kutoka UGANDA,    KENYA na TANZANIA,-   LVRLAC.
Katika hotuba yake ya ufunguzi kwa niaba ya rais JAKAYA KIKWETE, kanali MASSAWE amewakaribisha Wajumbe kutoka KENYA na UGANDA, pamoja na Halmashauri zinazozunguka Ziwa Victoria,Huku akiipongeza LVRLAC kwa mafanikio na kutoa ushauri kwa umoja huo.
Takriban Washiriki  450  wakiwemo  Wakurugenzi wa Halmashauri, Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri 28 za Tanzania wanahudhuria  mkutano huo, ambao unafanyika  katika viwanja vya GYMKHANA, katika  manispaa ya BUKOBA.
 Picha juu ni katika kuimba nyimbo za mataifa shiriki.

Washiriki wa Mkutano huo, jana, walishiriki katika shughuli za hifadhi mazingira na upandaji miti katika  maeneo mbalimbali ya Manispaa ya BUKOBA.
Hatua hiyo  ni kuunga mkono jitihada za Mkuu wa mkoa wa KAGERA, kanali mstaafu FABIAN MASAWE.

Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI, bwana AGGREY MWANRI,  ambaye pia amehudhuria mkutano huo, anatarajia kuufunga  mkutano huo.
Kasibante fm Redio kama kawaida yetu tukarusha matangazo ya moja kwa moja kutoka viwanjani hapo.

No comments: