MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 30 October 2012

BOMU LA KILIPUKA KARAGWE NA KUUA

Watoto  sita wamefariki dunia na mwingine  kujeruhiwa  vibaya katika kijiji  cha RUGARAMA kata ya IHANDA wilaya ya karagwe  mkoani kagera bada ya kuripukiwa na kitu kinachosadikiwa kuwa  ni bomu.

Kamanda  wa polisi wa mkoa wa kagera   PHILIPO KALANGI  amethibitisha  kutokea  tukio hilo lililotokea asubuhi ya jumanne,ambapo  kati ya watoto waliopoteza maisha wapo waliokuwa wanafunzi wa shule ya msingi
 
Mwenyekiti  wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye ni mkuu wa wilaya ya karagwe darry rwegasila ambaye yupo katika eneo la tukio amesema kuwa wataalamu wa jeshi la wananchi wa Tanzania wamethibitisha kuwa hao waliopoteza maisha walikuwa wakichezea bomu ambalo limewalipukia.

Rwegasira amewataadharisha wananchi kuwa makini wanapookota vyuma chakavu na kwamba wanapohisi kitu chochote wasichokielewa ni muhimu wakatoa taarifa katika vyombo vya dora.
Uchunguzi zaidi juu ya tukio hilo bado unaendele.

No comments: