Rais wa Kenya Mwai Kibaki, amekataa
kuidhinisha mipango ya wabunge wa taifa hilo kujipatia kitita kikubwa cha pesa
kama marupurupu ya kuhudumu kama wabunge.
Wabunge hao walipanga kujilipa dola
alfu mia moja na kumi kila mmoja kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Lakini bwana Kibaki amesema kuwa
hatua hiyo inakiuka katiba na haiwezi kutekelezwa wakati ambapo walimu pamoja
na madaktari nchini Kenya wamekuwa wakigoma kudai nyongeza ya mishahara.
Waandamanaji waliojawa na ghadhabu
nchini Kenya walijitokeza hapo jana kulaani hatua ya wabunge hao kutaka
kujilipa mamilioni ya pesa kama pesa za ziada wakati bunge litakapofunga vikao
vyake kwa maandalizi ya uchaguzi mwaka ujao.
No comments:
Post a Comment