MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 31 October 2012

RAIS WA ZANZIBAR AMEFANYA UTEUZI MWINGINE KATIKA MWEZI WA KUMI

NA MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteua Amina Juma Zidikheir kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utumishi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar. 
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahya Mzee imesema kuwa uteuzi huo ameufanya kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 8(1) (a) cha sheria ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar namba 11 ya mwaka 2003. 
Amina Juma Zidikheri aliwahi kuwa Mhasibu mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kabala ya kustaafu kwake. Uteuzi huo umeanza tarehe 27 Oktoba,2012 

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012

No comments: