MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 2 November 2012

BREAKING NEWS!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa habari za hivi punde, wananchi wamechomewa nyumba zao wilwywni karagwe.


Habari kamili inasema kuwa ananchi wa kijiji cha Luita kata ya Rugu wilayani Karagwe  wamelalamikia utaratibu wa serikali ya wilaya hiyo unaotumiwa katika kuwahamisha katika baadhi ya maeneo  opereisheini inayoendeshwa katika sehemu mbalimbali za mkoa kagera.

Baadhi ya wananchi  niliofanya nao mahojiano, wameeleza zoezi hilo kutekerezwa kwa njia za vitisho ikiwa ni pamoja  na kuchomewa nyumba zao ambapo zaidi ya nyumba 20 zimeripotiwa kuchomwa moto mpaka sasa.

Miongoni mwa raia hao ni Kasiri Pascal aliyesema kuwa nyumba 16 zilizchomwa jana lakini naye Makaranga Makoye amethibitisha kuwa ni nyumba zaidi 20 hadi sasa, na wanasema kuwa pale kuna wanyambo, wanyarwanda na wasukuma lakini kwa mujibu wao wanaochomewa ni wasukuma.

Operesheni hiyo inaongozwa na mwenyekiti wa kijiji Silidion Mgenyi huku Polisi na Mgambo wakichoma nyumba bila kujali vifaa vya wananchi hao na hawana pa kulala hadi sasa.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya karagwe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya DARY  RWEGASIRA amesema zoezi hilo ni halali na linatekelezeka kwa misingi ya haki katika operesheni inayofanyika Karagwe, Muleba na Ngara.

No comments: