MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 15 November 2012

UZINDUZI WA MRADI WA WAENDESHA PIKIPIKI WILAYANI MISENYI MKOANI KAGERA.

 
 
Kamanda wa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani Kagera  Wiliam Nkonda ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa mradi wa waendesha pikipiki wilayani Misenyi mkoani Kagera.

Kamanda NKONDA amesema kuwa,madereva hao wakizingati hayo wananweza kupunguza ajali kwa kiasi kikubwa.

Aidha ameongeza kwa kuwataka madereva hao kuachana na  tabia ya kuhusisha pikipiki zao  katika matukio ya uharifu kwani baadhi ya  waarifu hutumia pikipiki hizo katika shughulki zao za uporaji.

Kamanda NKONDA amewaomba watumiaji wa usafiri wa pikipiki kuzingatia suala la uvaaji wa element kwa usalama wao kwani nao wamekuwa kikwazo kwa kupuuzia suala hilo.

Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoani hapa bwana WISTON KABANTEGA amewaombwa waendesha pikpiki kuzingatia mafunzo wanayokuwa wanapewa pamoja na sheria za usalama barabarni kwani takwimu zinaonesha ajali za pikipiki zinaongezeka mwaka hadi mwaka nchini.

Pia bwana KABANTEGA amewaombwa bodaboda hao kuacha tabia ya kutumia njia za mikato mikato kwa kupata vyeti vya kugushi ili wapate leseni kitu ambcho si sahihi na ni kosa la jinai hivyo hawana budi kuvitumia vyuo vya udereva ili kupata vyeti sahihi na hatimaye kupata leseni.

Mradi huo unaundwa na vikundi sita vyenye waendesha pikipiki 170 na madereva zaidi ya ishirini na nne kati yao wametukiwa vyeti vya mafunzo na leseni.

No comments: