MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 4 January 2013

BIASHARA YA MAGENDO KUSABABISHA UPUNGUFU WA PATO LA MKOA WA KAGERA

Mkuu wa mkoa wa Kagera kanali mstaafu FABIAN INYASI MASSAWE, amesema kuwa hadi sasa changamoto kubwa ya kushuka kwa mapato ya mkoa ni pamoja na biashara ya magendo hasa ya kahawa, sababu nyingine ni kuchelewa kupitishwa kwa sheria ya mapato kwa halmashauri. Hata hivyo kanali Massawe amesema kuwa tatizo lingine kupungua kwa ushru wa kahawa pamoja na uhaba wa wataalamu wa kilimo na maofisa ughani.
 Kanali Massawe amesema hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari, alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa serikali ya awamu ya nne.
 Katika mkutano huo mkuu huyo wa mkoa, amewataka vijana kuacha kutoa lawama kwa serikali, badala yake wajibidiishe kufanya kazi kwa kutumia nguvu zao wenyewe na serikali itaendelea kuwaunga mkono katika hilo.

MWANA HARAKATI

No comments: