MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 7 January 2013

BREAKING NEWS!!!!!!!!!!! POLISI WAUAWA TENA KAGERA

MWANA HARAKATITaarifa za awali zinasema kuwa makamanda wawili wa jeshi la polisi mkoani Kagera wameuawa na wananchi katika shughuli zao za utendaji kazi.

Taarifa za awali kutoka kwa kamanada wa polisi mkoani Kagera Kamishina msaidizi PHILIP KALANGI, vifo hivyo vimetokea baada ya polisi watatu wa kituo cha Benako wilayani Ngara, kujifanya wanunuzi wa meno ya tembo katika kijiji cha Lugu ili wawabaini wananchi wanaojihusisha na biashara hiyo, lakini baada ya kufanikiwa kuwapata wauzaji na kuwakamata, inasemekana zilipigwa simu kwa wananchi wengine na kukusanyika na wakaanza kupigana na polisi hao kwa kuwakata mapanga, huku wakiwawekea kizuizi barabarani na hatimaye wawili kuawa na mmoja kukimbia.

Tukio hilo linatokea siku chache baada ya polisi wengine wawili kuawa huko huko Ngara, jambo ambalo linaonesha kuwa hali si nzuri kwa kipindi kifupi mkoani humo.

Siku chache katika mkutano wa mkuu wa mkoa wa Kagera kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, mkuu huyo wa mkoa aliulizwa na waandishi habari kuhusu mkoa kuwa katika hali ya vurugu ambapo alisema kuwa kwasasa mkoa huko shwari, lakini tukio la leo linaonesha kuwa majibu ya mkuu huyo si sahihi.

No comments: