MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 16 January 2013

WATU WATATU WAUAWA KAGERA KWA KUTUHUMIWA KUWA NI MAJAMBAZI

Akiongea na waandishi wa habari mkoani Kagera, kamanda wa polisi mkoani humo kamanda Philipo Kalangi amesema kuwa majambazi walio huawa ni mioingoni mwa majambazi sugu ambao wamekuwa wakijiusisha na vitendo vya uhalifu ndani na nje ya mkoa kagera.
 Jeshi la polisi mkoa kagera limefanikiwa kuwaua majambazi watatu huku wengine wawili wakifanikiwa kukimbia hatua iliyofikia kufuatia opreisheni inayo endelea kufanywa na jeshi la polisi mkoani humu ikilenga kuwatia mbaroni watu wanao jiusisha na vitendo vya ujambazi mkoani humo.
Katika opreisheni hiyo kumekamatwa injini tanoza boti zenye thamani ya shilingi milioni ishirini bunduki tatu na risasi 25.

Pia jeshi hilo limekamata misokoto ya bangi na lita 120 za pombe aina ya gongo katika operesheni inayoendelea mkoani humo.


MWANA HARAKATI

No comments: