MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 11 February 2014

FURSA MKOANI KAGERA- RC AKARIBISHA WAWEKEZAJI


Mkuu wa mkoa wa kagera kanali mstaafu FABIAN  MASAWE amewataka wawekezaji wa nje na wa ndani kuja kuwekeza katika mkoa wa kagera kwani bado una fursa nyingi za uwekezaji katika mambo mbalimbali ya kiuchumi ,utalii,elimu afya pamoja na uvuvi.

Kanali amsawe ametoa rai wakati akiongea na waandishi wa habari .

Amesema kuwa katika mkoa wa kagaera bado kunahitajika uwekezaji katika zahanati ambapo mpaka sasa hivi mkoa wa kagera una jumla ya zahanati 269 vituo vya afya 30 na vituo vya afya kumi na tano.

Aidha kanali masawe ameongeza kuwa kutokana na umuhimu wa faya kwa wananchi wawekezaji hawanabudi kuongeza zahanati pamoja na hospital ili kuongeza upatikanaji wa huduma kwa karibu.

Kanali masawe ameongeza kuwa  katika kongamano hilo wamewashirikisha wawekezaji wa ndani na nje katika kusaidiana na serikali kutangaza furs zilizopo hapa mkoani kagera.

MWANA HARAKATI

No comments: