MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 11 February 2014

WAKAZI WA KIJIJI CHA MLODAA MKOANI DODOMA WAMETAKIWA KUJUA MGAWANYO WA HAKI NA USAWA KWA WANAWAKE NA WALEMAVU.



                  
 Akizungumza katika Mdahalo ulio andaliwa na asasi isiyo ya kiserikali (CHANGONET) Afisa tarafa wa wilaya ya Chamwino bwana Mohamed Mtaki amesema wananchi wanatakiwa kufahamu haki pamoja na usawa dhidi ya wanawake na walemavu.


Aidha bwana mtaki  amesema  katika jamii kunabaadhi ya makundi ambayo yanaamini kuwa wanawake hawana haki ya kumiliki na kusimamia  haki na  hiyo ni mila potofu katika jamii.

Nae afisa maendeleo ya jamii wilayani Chamwino Bi Jaina Msangi  amesema katika mgawanyiko wa rasiliamali wanawake wengi wamekuwa hawapewi kipaumbele licha ya kuwa  wao ni mchango mkubwa katika jamii.

Kwa upande wa  wananchi wa kijiji cha mlodaa wamekiri kuwepo kwa unyanyasaji wa   kijinsia katika kijiji chao na kusema kuwa  wanahitaji elimu ili  kubadilika.

 

MWANA HARAKATI

No comments: