MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 26 February 2014

MABILIONI YA PESA BUKOBA




Mkurugenzi Mtendaji wa BUWASA,  mhandisi Chaggaka Kalimbia amesema wateja elfu 87 katika manispaa ya Bukoba  wanatarajiwa kuunganishiwa huduma ya maji safi na Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira -BUWASA- ifikapo Juni mwaka huu,  baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji.


Amesema kuwa baada ya wateja hao  kuunganishiwa, watakuwa wanapokea maji kutoka kwenye tanki zilizojengwa eneo la Kashura na Magoti, na kuwa tanki hizo zitakuwa na uwezo wa kubeba lita milioni tatu na laki saba.

Mhandisi Kalimbia amefafanua kuwa  kufikiwa kwa wateja hao, matumizi ya maji katika manispaa ya Bukoba yataongezeka hadi kufikia lita milioni 11 laki mbili na elfu 37 kwa siku tofauti na lita milioni nane na laki mbili kwa sasa.

Amesema  kukamilika kwa mradi huo, kutawezesha  kuzifikia kata nne ambazo zilikuwa hazijafikiwa huduma ya maji safi na salama, ambazo ni Kagondo, Kahororo, Nyanga na Buhembe.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa hadi kukamilika kwa mradi huo zaidi ya shilingi   Bilioni 27 milioni 528   na laki tatu   zinatarajiwa kutumika.
                             

MWANA HARAKATI

No comments: