MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 3 February 2014

WANANCHI WAMETAKIWA KUTUMIA MASHIRIKA KATIKA MASUALA YA KISHERIA


Rai hiyo imetolewa mapema leo, na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, mheshimiwa GADDY MJEMMAS, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria Tanzania.
Jaji MJEMMAS amesema kuwa baadhi ya Watu wamekuwa wakipoteza haki zao kwa kukosa uelewa kuhusu masuala ya sheria, huku baadhi yao wakipoteza muda kwa kufungua mashauri mahakamani  yasiyostahili.

Akitolea mfano, Jaji MJEMMAS amesema kuwa mwananchi mmoja, ambaye hakumtaja jina, alifika mahakamani kwa nia ya kumfungulia kesi  ya madai baba yake mzazi ambaye bado yuko  hai, akimdai Mirathi.

Amesema kuwa Mirathi hutolewa kwa kuzingatia  matakwa ya mtoa Wosia, hivyo endapo mwananchi huyo angekuwa na uelewa wa  sheria, asingepoteza muda wake kufika mahakamani.

Jaji MJEMMAS pia amewataka Wananchi mkoani KAGERA kushirikiana na Polisi pale unapofanyika upelelezi kwa makosa ya jinai, na pia wajitokeze kutoa ushahidi mahakamani pale kesi inapoanza kusikilizwa.

Maadhimisho ya Siku ya Sheria Tanzania huashiria kuanza kwa Mwaka wa  shughuli za  Mahakama nchini.

Kauli Mbiu ya Mwaka huu ni : ‘UTENDAJI HAKI KWA WAKATI: UMUHIMU WA USHIRIKI WA WADAU’.
MWANA HARAKATI

No comments: