MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 16 March 2014

BASI LA TIMU YA YANGA LAPATA AJALI MOROGORO


      Tazama picha chini baada ya basi hilo kunyanyuliwa upande mmoja                       
Gari hilo likionekana upandeni
Basi hilo kwa mbele
Basi la timu ya Young Africans lililokuwa limebeba wachezaji pamoja na viongozi wa benchi la ufundi limepata ajali eneo na Mikese Mizani mkoani Morogoro baada ya Mabasi yaliyokua yakitanua kuelekea mikoa ya bara kuziba njia na kusababisha kutumbukia kwenye mtaro.

Basi hilo limepata ajali likitokea mkoani Morogoro kwenda Dar es Salaam baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro jana.

Taarifa zinasema Katika ajali hiyo iliyotokea majira ya saa tatu na nusu asubuhi hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa na kwa sasa timu inaondoka na usafiri wa basi jingine kuelekea jijini Dar es salaam.

Na Mwanaharakati.

No comments: