MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 8 March 2014

WAKUU WA MIKOA KUTOKAA OFISINI

Kamati za ulinzi na usalama katika mikoa ya Kagera na geita, zimetakiwa kulinda vituo vya dawa na kufuatilia jinsi zinavyopokelewa na kusambazwa kwa umakini.              
Bohari iliyozinduliwa
Hatahivyo wakuu wa mikoa hiyo wametakiwa kufuatilia kwa karibu, bila kusubiria ofisini ili wajiridhishe na jinsi utaratibu unavyofanyika kwani kuna wizi mkubwa wa dawa za serikali katika mikoa hiyo.
Hayo yamesemwa na naibu waziri wa afya Dk KEBWE STEPHEN KEBWE, katika uzinduzi wa bohari ya huduma ya vifaa ba dawa kwa mikoa ya Kagera na Geita, iliyozinduliwa katika eneo la MALAHALA wilayani Muleba mkoani Kagera, itakayohudumia jumla ya vituo 270.

Amesema kuwa serikali inasikitika kuona dawa za serikali zinapatikana kwenye vituo vya watu binafsi, huku wananchi wakikosa huduma katika hosptali za serikali, hasa wilaya ya Ngara ikiongoza kwa upotevu wa dawa.
Naibu waziri STEPHEN KEBWE akikata utepe

Naibu waziri akipata maelezo ndani ya Bohari hilo
Kaimu mkurugenzi MSD COSMAS MWAIFYA
 
Kwaupande wake mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa bohari ya dawa nchini, Profesa ALI MTULIA, amesema kituo hiki kitahudumia vituo vyote vya afya mkoani Kagera, na baadhi ya wilaya za Chato, Bukombe na Mbogwe, mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Bodi ya bohari ya dawa Profesa ALI MTULIA


Awali, bohari ya mwanza ilikuwa ikihudumia mikoa 6, halmashauri 37, vituo vya afya na zahanati  elfu moja  na 73.

Na Mwanaharakati.

No comments: