MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 7 March 2014

MAKAHABA WAENDELEA KUKAMATWA DODOMA

JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA LIMEENDELEA KUFANYA MSAKO KATIKA MAENEO MBALIMBALI NA KUFANIKIWA KUWAKAMATA WANAWAKE 15 WANAOJIHUSISHA NA BIASHARA HARAMU YA KUUZA MIILI YAO.
 Akithibitisha kukamatwa kwa wanawake hao Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime amesema wanawake hao wanatoka Mikoa mbalimbali nchini  na Msako wa kuwakamata  umefanyika   March 05 mwaka huu majira ya saa tatu usiku  katika mitaa ya uhindini na Air Port.



Aidha  Kamanda Misime amesema kuwa katika msako huo watu wawili wanaume wamekamatwa wakiwa na mirungi robo kilo katika mtaa wa barabara ya nane Manispaa ya Dodoma ambao ni NASSOR ALLY mwenye miaka 45, Mwarabu mkazi wa barabara ya kumi na AYUBU TEPO mwenye miaka 40, Muarusha, Fundi cherehani mkazi wa Chamwino.

Pia katika Wilaya ya Kongwa kijiji cha Mlanje kata ya Matongoro  amekamatwa mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la SHEDRACK MACHILE mwenye miaka 46, akiwa na Lita 30 za pombe ya moshi akiziuza.

Kamanda Misime amesema msako unaendelea na amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.

Na Mwanaharakati.

No comments: