MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 15 March 2014

BREACKING NEWS!!!MATOKEO YA SASA JIMBONI KALENGA YASHANGAZA


Ni baadhi ya wananchi wakitafuta majina katika vituo vya kupigia kura.

Baadhi ya Wanakijiji cha Kalenga A,kata ya Kalenga Iringa Vijijini mkoani Iringa wakiendelea kupiga kura kumchagua Mbunge wamtakaye wa jimbo hilo la Kalenga.
Baadhi ya akina Mama waliojitokeza kupiga kura mapema leo asubuhi katika kijiji cha Kalenga A,kata ya Kalenga Iringa Vijijini wakitazama majina yao kwenye ukuta tayari kwa kutumia haki yao ya msingi ya kumchagua kiongozi wamtakae kwa kupiga kura
Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo unafanyika leo,ambapo vyama Vitatu;CCM,CHADEMA na CHAUSTA vikiwa vimesimamisha wagombea wake katika uchaguzi huo unaotokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo,pia Waziri wa Fedha,Dk William Mgimwa.

Aidha Wagombea wa Chadema Grace Tendega na wa CCM,Godfrey Mgimwa ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kuchuana na hatimaye mmoja wao kuibuka kinara kwa kupigiwa kura na Wananchi,huku mgombea wa CHAUSTA,Richard Minja akipewa nafasi ndogo kutokana na maandalizi hafifu ya ushiriki wake.
                                    Na Mwanaharakati.

No comments: