Mohammed Musa Yusufu maarufu kama Mwarami,
anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na sare pamoja na kutapeli watu
kwa kuuza fomu feki za kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Anasema “Mdogo wetu Omari alikuja nyumbani na kutuambia amekutana na mtu anayehusika na fomu za kujiunga na Polisi na kwamba zinauzwa kwa shilingi 250,000. Kwa kuwa hakuwa na hela, aliamua kuuza kitanda na godoro na fedha zingine akaongezewa na mama,” alisema mmoja wa dada wa kijana aliyetapeliwa, aliyejitambulisha kwa jina la Siwa.
Alisema baada ya kupata kiasi hicho,
Omari alimfuata mtu huyo akiwa na rafiki yake aitwaye Ali Kassimu ambaye naye
alitaka kununua fomu hiyo.
Baada ya kumpatia, walipewa fomu
hizo na kuelezwa kuwa walitakiwa kusafiri kuelekea Tanga sehemu iitwayo Kibuku
ambako ndiko ilipo kambi yao.
Walipofika huko, waliulizwa kuhusu
zilipo fomu za kujiunga, lakini walipowaonyesha, askari waliokuwepo kambini
hapo walizibaini kuwa hazikuwa halisi, hivyo vijana hao waliwekwa chini ya
ulinzi ili kusubiri taratibu zingine kufuatwa.
Ni kwa hisani ya EDDY.
Ni kwa hisani ya EDDY.
No comments:
Post a Comment