MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 29 March 2014

MAKAMU WA RAIS NA WAZIRI MKUU PINDA, AONGOZA MAZISHI YA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA MARA

Yamefanyika leo, kwao wilayani KILOSA mkoani Morogoro.


Waziri mkuu Pinda akiweka udongo kwenye kaburi, hapo Kilosa

Waziri mkuu Pinda akimfariji mzee Gabriel Tupa, baba mzazi wa aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Mara John Gabriel Tupa, baada ya mazishi.
Mazishi hayo yameongozwa na makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dk.MUHAMED GHARIBU BILARI na kuudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo waziri mkuu MIZENGO PINDA na waziri wa nchi ofisi ya rais mahusiano na uratibu bw.STEPHANO WASIRA.


Bwana TUPPA alifariki ghafla Machi 25, mwaka huu, akiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime, JOHN HENJEWELE, wakati akipokea taarifa ya wilaya ambapo alitarajiwa kuweka jiwe la msingi katika jengo la kusaidia matatizo ya ardhi na kushiriki ufungaji wa mafunzo ya mgambo.

Mwili wa marehemu Tuppa,uliagwa jana na maelfu ya wananchi wa mkoa wa Dodoma kabla ya kuelekea KILOSA, mkoani Morogoro kwa ajili ya mazishi.
Wakati wa uhai wake, marehemu Tuppa aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya za Chunya, Mwanga, Bukoba, Muleba na Dodoma, kabla ya kupandishwa cheo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara mwaka 2011.

Marehemu Tuppa alizaliwa Januari mosi, 1950 wilayani KILOSA, mkoani Morogoro, ameacha Mjane na Watoto Watano.

Na Mwanaharakati.

No comments: