MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 25 March 2014

VURUGU ZA JANA MASAI WAKIGOMA KUTOKA UWANJA WA NDEGE



LEO majira ya sita mchana hadi saa kumi na moja jioni katika barabara iendayo uwanja wa ndege wa kimataifa KIA Kilimanjaro International Airport kumetokea machafuko pata shika vuta nikuvute shati kuchanika rubega kufumuka..!

Takribani kama masaa mawili usalama ulipotea baada ya Wamasai kudai kufukuzwa katika makazi yao wakiambiwa ni eneo la uwanja wandege.

Wamasai hao waliamua kuzuia magari yalioelekea Uwanjani hapo huku wakisema kuwa hata wamiliki wa uwanja huo nao wahame kwani waliwakuta awali wakiishi hapo.

 Polisi na magari ya PT walifika katika tukio hilo na kutaka kumaliza migogoro hiyo kisheria ila wamasai wamesema endapo muafaka utalenga kuwakandamiza hawako tayari kuhama.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: