MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 7 April 2014

20% APELEKWA KWA MGAGA


Abas Kinzasa ‘20%’, anadaiwa kunaswa laivu akiwa kwa mganga wa kienyeji akipata tiba ya kupunguza na kuondoa sumu ya utumiaji wa bangi na pombe

Ni katika kijiji cha Ngukumo mkoani Tabora baada ya mameneja wa wasanii wa Bongo Fleva, Papa Misifa na Steve Mbaga kumshika mkono 20% na kutafuta mganga wa kienyeji ambaye aliwatangazia kuwa ana dawa zinazoweza kumuondoa sumu hiyo.

Mameneja hao ambao walisema walilazimika kufanya hivyo ili waweze kumrudisha 20% kwenye gemu kwa mara nyingine kwani bado wanaamini ana uwezo mkubwa kwenye muziki wa Bongo Fleva.

“Kiukweli mimi na mwenzangu tumekuwa tukisikitishwa kwa muda mrefu baada ya 20% kubobea kwenye matumizi ya pombe na bangi na hasa alipozidiwa hadi akashindwa kufanya muziki huu ambao tunaamini kwake ndiyo ilikuwa ajira pekee.

“Kwa kutambua hilo tulimtafuta na kuongea naye, alipokubaliana nasi tukaamua kumpeleka kwa mganga wa kienyeji, ameshapata tiba na tayari ameonyesha kujitambua, hivyo hivi karibuni tunaanza kufanya naye kazi na ndiyo tunatoka kumlipia nyumba ya kuishi maeneo ya Mwananyamala Hospitali,” alisema Papa Misifa.

Kupitia (Ijumaa Wikienda) nilipopata story hii, lilimtafuta 20% ambaye mwaka 2011 alichukua tuzo tano za Kili alipozungumzia suala hilo “Ni kweli Papa Misifa na Steve Mbaga wamejitahidi sana kunifanya niachane kabisa na matumizi ya pombe maana walinipeleka kwa mganga wao ambaye kweli amenisaidia.

“Ujue kilichokuwa kikiniyumbisha siku zote hizo ilikuwa ni pombe maana bangi ilikuwa si kiivyo, nilipokuwa nakunywa pombe kweli ilikuwa ikinitoa kwenye njia na kunifanya kujiona mimi ndiyo mimi kiasi cha kushindwa hata kuwaheshimu wenzangu na ndiyo jambo pekee ninaloweza kusema limenifanya kuwa hivi.”

Na Mwanaharakati.

No comments: