| Mkuu wa kituo cha Polisi Kahama Elias Haway |
Haway alipohojiwa
amekiri kutokea kwa ajali hiyo huku alisema kuna upotoshaji mkubwa wa taarifa
hiyo kwani yeye ndiye aliyegongwa na mwendesha pikipiki huyo wa kwanza.
Amesema alipotaka
kusimama kumwona mtu huyo aliyegonga, aliona watu wameanza kumzonga naye
akamua kukimbia kwa usalama wake ndipo alipoweza kuwagonga tena wale wengine
wawili.
Mganga Mfawidhi wa
Hospitari ya wilaya ya Kahama Dk Joseph Foma amethibitisha kugongwa na gari
watu hao na wamelazwa katika wodi namba moja katika hospital hiyo, huku hali
zao zikiwa mbaya na kwamba wapo katika utaratibu wa kumuhamishia Malugu katika
hospitali ya Bugando Jijini Mwanza.
|
Msukuma Toroli Fitina Majuto akiwa
Hospitalini Hapo
|
|
Mtembea kwa
miguu Cosmas Peter akiwa hoi hospitalini
|
Ajali hiyo imetokea Jana
majira ya 1.30 usiku katika barabara itokayo isaka kuingia kahama mjiniu ambapo
Haway akiendesha gari yake Toyota Rav 4 lenye namba T
798 BSK alimgonga mwendesha pikipiki.
Watu waliogongwa
wametambuliwa kwa majina ya Joseph Malugu (35) mkazi wa Mbulu Bw.
Fitina Majuto (20) na Cosmas Peter (21) wote wakazi wa mjini hapa mitaa
ya Nyasubi mjini Kahama.
Mashuhuda wa tukio hilo
wamesema Haway alianza kumgonga mwendesha bodaboda Bw. Malugu katika eneo la
Zahanati ya Igalilimi ambapo watu wenye
hasira walimzingira wakimtaka asimame naye akakimbia huku akiwagonga
tena waenda kwa mguu wawili.
Wamesema Haway
akionekana kuwa amelewa hakutaka kuwatii watu waliyokuwa
wakimweleza ndipo alipoondoa gari
lake kwa mwendo kasi na kwenda
kumgonga Bw. Majuto katika eneo
la Mkude ambae aliumia sana kwenye sehemu ya tumbo na
kusababisha utumbo kutoka nje.
Shuhuda mmoja
Mkulo Iddy amesema eneo hilo pia Haway hakutaka kusimama na aliendelea na
mwendo kasi ndipo alipokwenda kumgonga mtu mwingine wa
tatu Bw. Peter katika barabara ya eneo la Paradise mitaa
ya Nyasubi.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment