MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 12 April 2014

TAARIFA KAMILI KUHUSU MELI YA MIZIGO ILIYOZAMA ZIWA VICTORIA

Watu kumi 10 wamenusurika kifo baada ya boati ya mizigo MV matata iliyokuwa imesheeni tani 280 za sukari ikitoka mkoani kagera kuelekea mkoani mwanza kuzama katikati ya ziwa Victoria.

Kuzama kwa boti hiyo yenye nambari za usajili MV 1105  mali ya KITANO CHACHA BUNANKA kumefuatia hali mbaya ya hewa katika ziwa Victoria.

Akizungumzia tukio hilo bwana KITANO ambaye ni mmiliki wa boti hiyo amesema watu hao 10 wamenusurika kwa kutumia boti za dharula zilizokuwemo ndani ya boti hiyo.

Kwa mujibu wa Kitano Boti hiyo MV matata ilianza kufanya zake katika ziwa Victoria toka mwaka 2010 ambapo mpaka inazama imehudumu kwa muda wa miaka mitatu tu katika ziwa hilo.

Kamanda wa polisi mkoa kagera GORGE MAYUNGA alipo hojiwa juu ya tukio hilo amesema kuwa amesikia tukio hilo lakini hana taarifa rasmi na kusema kuwa uenda limetokea katika ziwa Victoria upande wa mkoa wa Mwanza.
Na Mwanaharakati.

No comments: