Watu watatu akiwemo afisa
kilimo na mifugo wa kata, mwenyekiti wa kijiji na mwanakijiji mmoja, wameuawa
na wananchi wenye hasira kali baada ya kupigiwa yowe kuwa wezi wa mifugo.
![]() |
| Rpc Kagera George Mayunga |
Mwenyekiti
wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kyerwa ambaye pia ni mkuu wa wilaya
hiyo BENEDCT KITENGA, amesema kuwa mauaji hayo yamefuatia msako wa wizi wa
mifugo uliofanywa na viongozi wa kijiji cha Kitale ili kubaini mifugo iliyokuwa
imeibiwa katika kijiji hicho kwa muda wa wiki moja iliyopita.
![]() |
| Dc Kyerwa Benedict Kulikila Kitenga |
Kwa
mujibu wa KITENGA viongozi hao walifika
katika kijiji cha Kalongo wakitokea kijiji cha Kitale na kuwakuta ng’ombe
waliokuwa wakiwatafuta baada ya kuibiwa katika kijiji hicho, kwa bwana Joas
Augustino mkazi wa kijiji cha Kalongo.
Baada
ya kuwakuta ng’ombe hao 12, waliamuru kuondoka na mtuhumiwa wa wizi wa ng’ombe
hao bw.Augustino, ili kumfikisha katika mikono ya sheria kwa mujibu wa taratibu
na kanuni za nchi.
Hata
hivyo inadaiwa kuwa baada ya kuondoka na mtuhumiwa huyo nyumbani kwake mke wa
mtuhumiwa alipiga yowe kuwajulisha wanakijiji cha Kalongo kuwa mmewe ametekwa
na kuchukuliwa na majambazi.
Kufuatia
yowe hilo lililo ambatana na ngoma ya kuashiria hatari, wanakijiji katika
kijiji cha Kalongo walibeba silahaa mbalimbali ikiwemo mapanga na kuwanyatia
viongozi hao waliokutwa wakiendelea na safari na kuwashambuliwa.
Katika maelezo ya baadhi ya
wanakijiji hao wanadai kuwa, askari mgambo baada ya kuona kundi lao wanazidiwa
nguvu, alikimbia kwa kujivuta vuta kutokana na madai kuwa alikatwa mguu ambao
umesalia katika eneo la tukio, na mpaka sasa bado hafahamiki aliko.
Akizungumza tukio hilo kamanda wa polisi mkoa Kagera Gorge Mayunga
amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo, na kuwataja waliouwa kuwa ni Shimbwilo Jonathan (44) Juma Mbogo (48)
na Jacknus Wamara (48) aliyekuwa afisa
kilimo na mifugo kata ya Bwile.
Aidha ameongeza kuwa tayari
jeshi la polisi limewatia mbaroni watu wanne kwa ajili ya kusaidia upelelezi wa
mauaji hayo, huku msako mkali ukiendelea ili kuwabaini wote walio husika katika
tukio hilo.
Akizungumzia suala la
kufanyika msako wa wizi usiku katika kijiji tofauti lililo zua tafsiri tofauti
miongoni mwa wakazi wa mkoa Kagera, kamanda Mayunga amesema kuwa ni vigumu
kuwalazimisha watu kufanya shughuli zao usiku ama mchana, ilimradi wafuate
taratibu za kutoa taarifa kwa ngazi tofauti za uongozi katika sehemu husika.
Miili ya marehemu hao watatu
imehifadhiwa katika Dispensary ya Nkwenda ikisubiri mazishi yanayotazamiwa
kufanyika keshoo (april 13) huku idadi kamili ya ng’ombe waliokuwa wakitafutwa
ikiwa bado haijafahamika.


No comments:
Post a Comment