![]() | ||
| Kushoto picha ikionesha mafuriko Dar es salaam, kulia Scaveter katika ukarabati daraja Goba |
Kutokana na mvua zinazonyesha hivi sasa kwenye jiji la Dar
es salaam pamoja na kusababisha mambo mengi kusimama, miundombinu kuharibika
hasa madaraja yanayounganisha njia kuu, pia zimesababisha vifo vya watu 10.
Nyumba nyingi zimeingia maji hasa maeneo ya mabondeni na
kulazimisha familia kuhama kutoka kwenye makazi yao ambapo mpaka sasa Polisi
Dar es salaam inasema watu kumi waliofariki, wamo watoto watano na watu
wazima watano.
Kamanda Suleiman Kova wa kanda maalum ya Dar es salaam
amesisitiza hali sio nzuri hivyo wananchi wanatakiwa wachuke tahadhari kwenye
makazi yao na hata wanaotembea na magari barabarani kwa sababu njia nyingi zina
mashimo na pia watu wapunguze mizunguko isiyo lazima barabarani.
| Hali ya daraja wakati limebomoka |
Wakazi
wa eneo la Mapinga Mkoani Pwani wameshindwa kuvuka Daraja la Mto unaokatisha
kwenye eneo hilo baada ya kutokuwepo kwa mawasiliano ya barabara kwa kukatika
kwa daraja hilo kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo
mbali mbali hapa nchini.
Akithibitisha kutokea kwa hitilafu hiyo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Ulrich Matei amesema ni kweli kumetokea kwa tatizo hilo na amewataka watumiaji wa barabara ya Bagamoyo kubadilisha njia na kuwanza kutumia barabara ya Morogoro mpaka hapo daraja hilo litakapofanyiwa matengenezo.
Wakati jitihada zikifanyika kurudisha mawasiliano ya barabara na makamanda wakitafakari juu ya kuweka daraja la muda, watu wameanza lawama eti mkandarasi. Lakini ukweli ni mambo ni matatizo yetu wenyewe.
Na Mwanaharakati.
Akithibitisha kutokea kwa hitilafu hiyo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Ulrich Matei amesema ni kweli kumetokea kwa tatizo hilo na amewataka watumiaji wa barabara ya Bagamoyo kubadilisha njia na kuwanza kutumia barabara ya Morogoro mpaka hapo daraja hilo litakapofanyiwa matengenezo.
Wakati jitihada zikifanyika kurudisha mawasiliano ya barabara na makamanda wakitafakari juu ya kuweka daraja la muda, watu wameanza lawama eti mkandarasi. Lakini ukweli ni mambo ni matatizo yetu wenyewe.

No comments:
Post a Comment