![]() |
| Mkuu wa mkoa Geita Magalula Said Magalula |
Agizo la kukamatwa kwa watendaji hao
limetolewa juzi na mkuu wa mkoa wa Geita Bw Said Magalula kwenye kikao kilichofanyika
katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Geita lengo likiwa kubaini ni watoto
wangapi waliofaulu na hawajaenda shule na watoro sugu.
Bw Saidi aliongeza kuwa kuna wazazi
ambao watoto wamefaulu kwenda sekondari lakini wazazi wanawaficha majumbani kwa
ajili ya kuwafanyisha kazi mbalimbali na ikiwemo kuwaozesha kwa nguvu au kuwapeleka
migodini kuchenjua dhahabu na wengine kuwapeleka kuchunga wakati kikao cha mkoa
kiliagiza watendaji wa kata zote wanatakiwa kuwakamata wazazi waliofanya hivyo
na kuwafikisha mahakani lakini mpaka sasa ni wazazi wachache waliotekeleza
hilo.
Bw Saidi akaagiza kuwa kati ya kata
35 kwenye wilaya Geita ni kata 20 tu zilizotekeleza agizo hilo la kuwakamata
wazazi na kuwafikisha mahakamani hivyo kuamuru watendaji 15 waliokataaa
kutekeleza agizo hilo kuhakikisha wanakamatwa mara moja na kufikishwa
mahakamani.
Lakini pamoja kukamatwa kwa
wetendaji hao mwandishi wa habari hii aliongea na mmoja wa watendaji ili
kutaka kujua kwanini walikiuka agizo la mkuu wa mkoa , Bw Wiliam Rufungu
ambambeye ni Mtendaji wa kata chigunga alisema kuwa kwenye kata yake
amekuwa na changangamoto kubwa kutokana na wazazi kuwaamisha watoto na
kuwatorosha kwenda nje ya kata yake.
Na Mwanaharakati.


No comments:
Post a Comment