Nicolaus Mac (None Association Movement) KWA MATANGAZO YA REDIO NA TV WASILIANA NASI KWA +255767814844- nicolausngaiza@gmail.com.
Tuesday, 20 May 2014
MAZISHI YA MSANII ADAM PHILP KUAMBIANA
Nyota wa filamu aliyefariki dunia ghafla Jijini Dar es Salaam, Adam Philip Kuambinana, anatarajiwa kuzikwa leo Jumanne kwenye makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Kwa Mujibu wa mratibu wa shughuli hiyo ya mazishi Steve Nyerere, Mwili wa Marehemu Adam Philip Kuambiana utapelekwa viwanja vya Leaders leo Jumanne kwa ajili ya wadau ndugu jamaa na marafiki kuuaga kabla ya maziko.
Marehemu Kuambiana alifarki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali ya Mama Ngoma Mwenge Dar es Salaam baada ya kuanguka akiwa kwenye upigaji picha filamu katika hoteli moja iliyopo eneo la Sinza.
Inadaiwa kabla ya umauti kumfika marehemu alikuwa akilalamika maumivu ya tumbo.
Mungu ailaze roho ya Marehemu Adam Kuambiana mahali pema peponi Amina.
Na Mwanaharakati.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment