MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 2 June 2014

NEWS ALERT!!!MAUAJI NGARA; SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UUZAJI WA POMBE USIKU


SERIKALI Wilayani Ngara mkoani Kagera imepiga marufuku uuzaji wa pombe nyakati za usiku baada ya kukithiri kwa matukio makubwa ya kuhatarisha usalama wa wananchi yakiwemo  ya watu kubakwa na kujinyonga.

 Mkuu wa wilaya ya Ngara Costantine Kanyasu ametoa agizo hili leo June 2 kwa watendaji wote wa vijiji na kata wilayani humo kufuatia matukio ya watu kujinyonga kuongezeka na kuhatarisha mtafaruku wa kiusalama.

Kanyasu amesema kuwa zaidi ya watu 10 wilayani humo kwa mwezi mei wamefariki kwa kujinyonga huku matukio matatu ya ubakaji yakitokea ambapo watu watatu wamefikishwa mahakamani kwa kujaribu kujinyonga.

Amesema wanaofanya na kufanyiwa matukio hayo wamekuwa wakitokakwenye vilabu vya pombe nyakati za usiku  na wengine wamepoteza maisha kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ugumu wa maish.

Pamoja na agizo hilo amevitaka vyombo vya ulinzi kuhakikisha vinavunja vilabu vya pombe ambavyo vitakaidi amri ya serikali kwa kuwafungia wateja ndani huku wakiendelea na biashara ya kuuza pombe usiku.
 Na Mwanaharakati.

No comments: