MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 21 August 2014

JAMII YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA HASA MIJI KWA KUFANYA USAFI



Warembo 18 kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wanashiriki mashindano ya Taji la Miss LAKE ZONE  mwaka 2014 wametembelea kituo cha watoto yatima cha Moyo wa Huruma kilichopo mtaa wa Mbugani Wilayani Geita mkoani humo na kutoa misaada mbalimbali yenye thamani ya shilingi laki 350,000/=, na wameonekana mfano wa kuigwa kwa kufanya usafi katika mji wa Geita.

Wakizungumza na mtandao huu, wamesema kuwa wameamua kufanya usafi katika mji huo ikiwa ni kutekeleza agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo Omary Mangochie, ya kuweka mji katika hali ya usafi kwa kufanya usafi kila Alhamisi.

Mamiss hao  wamemshukuru mdhamini wao Leonard Bugomola, ambaye ametoa vyumba 10 vya kulala, kila chumba ikiwa ni shilingi 80,000/=  kwa kila siku,  na chakula  chenye thamani Tsh 15,000 kwa kila mshiriki huku wakiishi  hotelini kwake kwa siku kumi wakiwa kwenye mazoezi. 

Mdhamini huyo Leonad Bugomola ambaye ni mfanya bishara mkoani humo, amesema kuwa ameamua kutoa zawadi hizo kutokana na Mungu kumjalia alivyo navyo na kuwa na kipaji cha kupenda michezo mbalimbali.

Bugomola aliwaomba wafanya biashala wenzake  wa mkoa wa Geita kujitolea kwa kudhamini Mamiss na kuacha Dhana ya kuwa Umiss ni uhuuni kwani Umiss ni ajira kama ajira zingine.

Shindano la kumpata Miss Lake Zone, litafikia tamati mwishoni mwa mwezi huu wa nane (8), mbapo mshindi wa kwanza atajinyakulia zawadi ya Gari.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: