Mahujaji wa Dini ya Kiislamu mkoani Kagera
wanaotarajiwa kwenda HIJJA, wametakiwa kufuata utaratibu utakaowekwa na Wizara
ya afya baada ya kuibuka kwa ugonjwa wa Ebola katika nchi za Afrika ya
Magharibi.
Shekhe
wa mkoa Kagera HARUNA KICHWABUTA,
amesema kuwa mahujaji wanatarajiwa
kwenda SAUD ARABIA katika mji wa MAKKA kwa ajili ya hija Septemba 25
mwaka huu.
Shekhe KICHWABUTA amesema kuwa kabla mahujaji hao
kuondoka watatakiwa kufuata utaratibu utakaowekwa na serikali kupitia Wizara ya
Afya ili kuepukana na hadha zinazoweza kujitokeza.
Amesema
kuwa serikali kwa kushirikiana na nchi nyingine bado wanaendelea kulifanyia
kazi suala hilo baada ya kuibuka kwa ugonjwa huo na hivyo kuwataka MAHUJAJI
kuendelea kujiandikisha na kulipa gharama za usafiri.
Kadhalika
Shekhe KICHWABUTA amewataka mahujaji hao
kufuata maelekezo ya mtume MUHAMAD katika kutekeleza nguzo hiyo muhimu ya
Uislamu.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment