MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 25 August 2014

NEWS ALERT!!! KIKAO CHA KWANZA CHA DHARURA MANISPAA YA BUKOBA CHAFANYIKA, BAADA YA MGOGORO WA MUDA MREFU

                                       
 Kikao hicho, kilichokutana chini ya Naibu Meya Alexander Ngalinda, madiwani hao mazungumzia hoja ya kutenga kata ili kufikisha huduma karibu na wananchi na kupendekeza majina yatakayotumika baada ya kutengwa kwa kata hizo.


Kata zinazopendekezwa kutengwa, ni kata ya Bakoba na kata ya Kashai, ambapo manispaa imetoa nafasi kwa watendaji wa kata kufanya tathmini ya kuweka mipaka katika maeneo yanayokusudiwa kutengwa.

Naibu meya Mh. Alexander Ngalinda, mkuu wa wilaya Bi Zporah Pangani katikati na mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Mh Balozi Khamis Kagasheki.
Kaimu mkurugenzi Robert Kwela akitaja Agenda za kikao hicho.

Mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi.  Ziporah Pangani, amewashukru wananchi wa manispaa hiyo, kwa kuwa wavumilivu wakati ambao vikao vilikuwa havifanyiki.
Bi. Pangani amewataka wananchi kuwa wamoja wakati wa kuanza kutekeleza masuala yaliyojadiliwa kwenye kikao hicho leo.

Nafasi aliyopangwa aliyekuwa meya wa manispaa ya Bukoba wakati huo Mh. John Aman
Baadhi ya madiwani na watalaamu wa manispaa ya Bukoba wakifuatilia kikao.


Baadhi ya viongozi watendaji wa manispaa ya Bukoba wakifuatilia kikao kilichoongozwa na naibu Meya Alexander Ngalinda.


Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA Bw. Shilejei, akisalimiana na katibu wa CCM manispaa ya Bukoba Bi Janet Kayanda aliyekumbatiwa amevaa nguo nyeus na kitambaa.

Waandishi wa habari wakiwa nje ya ukumbi wa manispaa ya Bukoba, baada ya kutoka nje wakati wajumbe wa kikao wakijadili hali ya awali ya mgogoro wa manispaa hiyo wakati huo.
Na Mwanaharakati.

No comments: