MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 20 August 2014

VIJIMAMBO!!! MAMA AMCHANA MTOTO SEHEMU YA HAKA KUBWA BAADA YA KUTOZALIWA NAYO

 
 




Mama mmoja ameamua kumchanja kwa Nyembe mwanae mwenye umri wa wiki mbili baada ya mtoto huyo kuzaliwa akiwa hana sehemu ya Haja kubwa.
Tukio hilo limetokea hivi karibuni baada ya mama huyo aliyefahamika kwa jina la Anastazia Ngilitu kumchana mwanae kwa wembe zaidi ya mara tatu ili kumsaidia kupata haja kubwa kwa kile kilichodaiwa mtoto huyo kuzaliwa akiwa hana sehemu ya haja kubwa.
Mama huyo mkazi wa Tabora aishie jijini Mwanza kwa sasa, amesema kuwa alijifungua watoto mapacha watatu ndani ya Mtaro  kisha wawili kufariki walipofikishwa Hospitali na kusalia mtoto mmoja aliyekutwa na tatizo la 
kukosa sehemu ya haja kubwa.

Sambamba na hayo,  mama huyo amesema kuwa  sababu za kumchana na mwanawe ni baada ya kumuona mtoto wake anashindwa kupata haja kubwa hali iliyosababisha tumbo kujaa upande wa kulia.

Katika hatua nyingine Mama huyo amesema kuwa kwa sasa hali yake ya Maisha siyo nzuri, kwani watoto wake wanaishi kwa kunywa maji na kwamba hapo awali alikuwa anafanya kazi ya kufua nguo kwenye nyumba za watu ila kwa sasa hawezi kutokana na kuwa na mtoto mdogo.

Sambamba na hayo mama huyu anasema kuwa licha ya kuolewa na wanaume watatu kwa wakati tofauti, na kila mmoja kumnyanyasa kwa kumpiga na mwingine kumdhurumu pesa, zaidi amesikitishwa na kitendo cha Mume wake wa sasa hivi  kumtaka kufanya mapenzi ikiwa tumbo la uzazi halijakaza, hali anayotaja kumsababishia maumivu makali na kutokwa na damu nyingi baada ya mumewe kumpiga.

Kitendo cha mama huyu kumchana mtoto wake kwa wembe  kinatoakana na hofu ya kwenda hospitali kwani anasema hana uwezo wa pesa kwani kwa sasa yeye mwenyewe anasumbuliwa na uvimbe katika titi lake la kushoto na alipoenda Hospitali ya SEKOTURE aliambiwa gharama za upasuaji ni shilingi elfu 30 na alipokosa alirudi nyumbani na kuendelea kujitibu kwa dawa za kienyeji.

Kwa upande wao baadhi ya majirani ambao wamekuwa wakimpa msaada mama huyu mara kwa mara,Wameiambia wanasema kuwa ana maisha magumu kwani mume wake humpiga na kumfukuza mara kwa mara hali inayomfanya aishi kwa kuomba omba na wakati mwingine kulala na watoto wake bila kula.


Na Mwanaharakati.

No comments: