MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 15 September 2014

HOT NEWS!!! OCS ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUPIGWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KWA KUTAKA KUBAKA



MKUU wa kituo cha polisi cha Nyamboge kilichopo katika kata ya Katoma Wilayani Geita Mkoani hapa amenusulika kupigwa na wananchi wenye  hasira kali  baada ya kukutwa akitaka kufanya mapenzi na mwanafunzi katika nyumba anayoishi mwanafunzi huyo.

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa tatu usiku ambapo wananchi wa kijiji hicho wakiwa na marungu na mikuki waliweka mtego wa kumnasa mkuu huyo aliyefahamika kwa jina Moja la Venance  kuwa ana tabia za kumrubuni mwanafunzi huyo kwa mda mrefu.

Aidha akizungumzia tukio hilo binti huyo  Rozimery Kahindi (17) anayesadikiwa kuwa mwanafunzi wa kidato cha nne alisema kuwa siku ya jumapili, mkuu huyo wa kituo alituma maaskari wawili wakaenda kumkamata huku akidai kuwa hajui hata kosa lake, lakini akalazimika kwenda na alipofika hapo alianza kulazimishwa kuwa anatembea na mwalimu wake, ndipo alipokataa na kulazimishwa kuandika maelezo ambayo hata yeye hayakumbuki hadi anakutana na wanahabari.

Aliendelea kusema kuwa baada ya kukataa kuandika maelezo alipelekwa rokapu na mda mfupi alifuatwa na askari mmoja kati ya wale waliomkmata kuanza kuandika maneno ya kutoa kichwani mwake na kulazimsha kusaini lakini aliendelea kugoma na alipigwa sana na kuamua kusaini kutokana na kutishiwa kufungwa na mara baada ya kusaini aliitwa na OCS huyo na kumwambia aende Nyumbani lakini arudi jioni ana shida naye ya muhimu sana lakini alaishindwa kurudi kutokana na kuchoka na kipigo alichokipata  kituoni hapo.

Kutokana na mkuu huyo wa kituo kutuhumiwa na mwanafunzi kuwa anamtaka kimapenzi ilibidi awaambie wanafunzi wenzake na wananchi na baada ya hapo wakatengeneza mtego ili wamnase.

Siku ya jumapili jana mkuu huyo wa kituo alikwenda Nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kuomba wafanye mapenzi kwa kuwa wenzake anaoishi nao hawakuwepo lakini aligoma kufanya hivyo, ndipo muda mfupi   wananchi waliokuwa wamemuona anaenda kwa binti huyo walifika hapo na kufunga mlango kwa nje na kuanza kupiga kelele na kumfanya OCS huyo kuvunja malango na kutoka nje lakini wanchi walifanikiwa kumkamta na kuanza kumpiga ambapo aliokolewa na askari  na kufikishwa  katika kituo kikuu cha polisi cha Wilaya ya Geita.

Diwani wa kata hiyo Josephat Komanya  alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kulaani vikali kitendo hicho na kuwaomba wanafunzi wa kata hiyo kuendelea kuwataja viongozi ambao wanawataka kimapenzi kwa nguvu.

Jitiada za kuzungumza na kamanda wa jeshi la polisi Mkoni hapa Joseph Konyo zinaendelea. 

Na.Valence,Robert,Geita.

 
Na Mwanaharakati.

No comments: