MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 16 October 2014

BREAKING NEWS!!!MALI ZA GGM ZA KAMATWA NA MAHAKAMA

Picha juu na chini ni moja ya Gari ya GGM aina ya Toyota Hiace yenye namba T258  BZP iliyokamatwa jana na Wakala wa Mahakama Kuu Mwanza na kuwekwa katika viwanja vya ofisi ya Madini ya Mkoa huo ili kupigwa mnada





Gari Moja ya Kampuni ya Uchimbaji wa Dhahabu Mkoani Geita (GGM)  imekamatwa na wakala wa mahakama kuu Mwanza na nyingine moja kukimbia baada ya kampuni hiyo kushindwa kulipa deni la zaidi ya Sh.57milioni.

Gari hiyo aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajili T258 ilikamatwa jana majira ya saa 7:00 mchana wakati gari hilo likiwa barabarani kueleka kazini huku dereva wa gari nyinyingine ambaye hakujulikana mara moja kutokomea kusikojulikana  baada ya kuwaona wakala hao wakikamata gari hilo.

Taarifa zinasema kuwa GGM ilishindwa kumlipa Peter Daudi kiasi hicho cha fedha ikiwa ni agizo la mahakama kuu  Mwanza iliyoitaka kampuni hiyo kumlipa stahiki zake  baada ya kushinda kesi namba 23 of 2014 iliyokuwa ikimkabili GGM kwa kumsimamisha kazi kinyela kwa tuhuma za wizi wa Mafuta.

 “Mimi nilikuwa mwajiliwa wa GGM, nimefanya nao kazi kwa muda wa miaka mitano ,ilipofika mwezi wa  nane mwaka  2012 nilisimamishwa kazi”alisema Daudi

Daudi alieleza kuwa baada ya kusimamishwa kazi aliamua kwenda mahakamani akisaidiwa na chama cha wafanyakazi Mgodini (TAMICO)  ambapo alishinda kesi na kutakiwa kurudishwa kazini na kulipwa  fedha zake zote za mshahara ndani ya siku 42 wakati akiwa nje ya kazi.

“GGM ilishindwa kunilipa ikabidi nirudi mahakamani kukazia hukumu,nikapata’ Court Broker’ wakala wa kukamata mali  ambao wamekamata magari gari moja na nyingine dereva amekimbia nayo  “alifafanua Daudi.

Pia Taarifa zinasema kuwa baada ya gari ya GGM kukamatwa Kampuni hiyo iliamua kulipa sh.15 milioni kiasi ambacho nikidogo na kwamba imelipa bila kufata utaratibu wa kimahakama huku kwani imeingiza fedha hizo kwenye account ya Mwajiliwa huyo.
Hata hivyo msemaji wa kampuni hiyo ambae ni meneja wa mawasiliano Tenga Tenga alipohojiwa juu ya tuhuma hizo alisema kuwa hana taarifa hizo kwani yuko nje ya kazi  na kuomba apewe muda ili aweze kufatilia suala hilo kisha atolee majibu.

“Niko nje ya Kazi naomba nifatilia alafu nitatoa majibu baadae baada ya kupata taarifa sahii toka ofisini”alisema Tenga……..

Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa chama cha wafanyakazi Wilaya ya Geita (TAMICO), Paternus Rwechungura ambaye alikuwa  anasimamia kesi hiyo alithibitisha kuwepo kwa kesi hiyo na kwamba mfanyakazi huyo alishinda kesi lakini GGM ikashindwa kulipa kwa muda wa siku 42 walizopewa na mahakama .

Baada ya kushindwa kulipa kwa muda huo aliamua kwenda kukazia mahakama na kesi hiyo ni meisimamai amimi mpaka leo hii mali ya GGM imekamatwa na ukamataji huo umezingatia thamani ya fedha anayodai.”alisema Rwechungula.
  Na Mwanaharakati.

No comments: