MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 20 October 2014

MSANII WA FILAMU BONGO AZUA KIZAAZAA BAADA YA KUTAPELIWA NA KAMPUNI YA USAMBAZAJI



Aisha Bui akiwa na jiwe lililotumika kuvunjia mlango wa kioo wa ofisi hizo.                                     


 Aisha alipofika ofisini hapo alishikwa na ghadhabu baada mhasibu wa kampuni hiyo kumwambia hakuwa na namba ya bosi wake wakati alijua akifika tu angepewa fedha hizo hivyo akashikana naye mashati na kuanza kuzipiga ambapo Aisha alisukumwa akadondoka pwaa!


Kitendo cha kusukumwa, kilimpandisha hasira Aisha na kuamua kuchukua jiwe ambalo lilishindwa kufungua mlango hivyo alichukua nondo na kuvunja mlango huo ambapo wafanyakazi walijifungia kwa ndani ili kumzuia asiingie ndani.



Wanahabari wa gazeti hilo walipomfuata  Ngeze kujua kulikoni kumtia mbaroni Aisha alisema alivamiwa na staa huyo na mabaunsa ambao walivunja ofisi pamoja na kushukua ‘laptop’ na fedha.

Mpaka kuchapisha taarifa hizi, Aisha na shemeji yake walikuwa bado wameshikiliwa na Polisi wa Kituo cha Maturubai, Mbagala.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: