MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 25 October 2014

NEWS ALERT!!!WAZAZI NA WALEZI MKOANI KAGERA KUWEKEZA KIDOGOKIDOGO ILI KUSOMESHA WATOTO WAO

 Naye mwalimu Tamim Kassi Suleimanambaye alikuwa mwalimu mkuu wa shule, amesisitiza kuwa lazima wahitimu kutambua kuwa wanapomaliza kidato cha nne ndiyo mwanzo wa masomo kwani sikuhizi huwezi kupata kazi bila kuwa na elimu ya juu.
Bw Wiliam Rutta akihutubia wageni na wahitimu shuleni Tweyambe


                                     






Wazazi na walezi mkoani Kagera, wameshauriwa kuendelea kuwawekea mazingira bora ya elimu watoto wao kutokana na mabadiliko ya kiwango kizuri cha elimu.

Kauli hiyo imetolewa na Tamim Kassi Suleiman katika mahafali ya shule ya sekondari Tweyambe wilayani Misenyi, akisisitiza kuwa kiwango cha kidato cha nne saizi hakiwezi kumletea muhitimu maendeleo kama hajajiunga kidato cha tano.

Amesema kuwa zamani aliyekuwa akimaliza kidato cha nne, angeonekana mtu mkubwa kwenye jamii kwasababu alifanikiwa kupata kazi sehemu yoyote, tofauti na sasa ambapo kila kazi inahitaji kiwango cha juu hivyo kutakiwa kuwa na elimu ya juu.

Mgeni rasimi katika mahafali hayo Bw Wiliam Rutta, amesema kuwa ni lazima elimu itengenezewe mazingira mazuri ili kuleta mafanikio, hivyo kama mwanafunzi wa zamani katika shule hiyo, atahkikisha anaedeleza mawasiliano ya kuitangaza shule hiyo, huku akisema kuwa kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali anaofanya nao kazi, watajitaidi kutatua tatizo la maji na masuala ya michezo shuleni hapo.

Wakati huo huo amewataka wazazi kutunzafedha kidogokidogo ili kiwasaidie kusomesha watoto pasipokutegemea misaada pekee.

Shule hiyo  ya sekondari Tweyambe, ina jumla ya wanafuzi wa kike na kiume 521, wakiwamao wa bweni 410  na 111 wa kutwa, ina walimu 22 ambao 19 wa kiume na 3 wa kike
 

Na Mwanaharakati.

No comments: