MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 24 October 2014

PONGEZI WILAYANI SENGEREMA HIZI HAPA


WANCHI wa Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza wamepongeza huduma  inayoedelea kutolewa na benk ya CRDB  kwa kuendelea kueneza huduma za ulipo tupo na Kuongeza ATM ili kupunguza usumbufu waliokuwa wakiupata.

Hayo yamebainishwa jana na baadhi ya  wananchi wa kijiji cha Kanyala katika Wilaya hiyo wakati benki hiyo ilipokuwa ikifungua huduma hiyo katika kijiji hicho na kusambaza huduma ya ulipo tupo kila kona.

Mwananchi mmoja ambaye ni mfanyabishara wa samaki Juma Masanja alisema kuwa kuwekwa kwa huduma hiyo kwani walikuwa wakihangaika sana kutunza pesa na kuchukua pesa lakini kuwekwa kwa huduma hizo wananchi wataacha kusumbuka.

Aliongeza kuwa wagonjwa wengi walikuwa wanahangaika pakutunzia pesa walikuwa wanatembea walikuwa wanatembea zaidi ya kilomita 15 kutafuta huduma hiyo kwahiyo kuwekwa kwa huduma hiyo ni mkombozi kwao.

Jamani tunashukuru benki hii kwa kuweka huduma kama hii kalibu na wananchi kwani tulihangaika sana kwa sasa benk ya CRDB Ni mkombozi wetu alisema.

Mkuu wa Wilaya hiyo Kareni Yunusu alipoulizwa juu ya huduma hiyo kwa wananchi wake alisema kuwa alitoa pongezi zake kubwa kwa benk hiyo na kuomba  mabenki mengine kuiga mfano kama huo wa CRDB.

Naye Meneja msimamizi katika Wilaya hiyo  ambaye ni  Leonce Matley wa Mkoa wa Geita alisema wameamua kutoa huduma hiyo kutokana na maombi ya wananchi wa kjijiji hicho na  wataenderea kushirikiana na wanachi kutoa huduma hiyo na watazidi kupeleka vijijini zaidi kwani ndiko bado wananchi wanahangaika sana kuliko mjini

Tuendelee kushirikiana sisi na ninyi wananchi  kwa kutoa huduma tunapokosea tunaomba mtuambie kwani tunataka kutoa huduma iliyo bora  na ukizingati biashara ni ushindani alisema Matley.

Na Mwanaharakati.

No comments: