MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 13 October 2014

WANANCHI WAVAMIA ENEO LA MWEKEZAJI GEITA, MWENYEKITI CCM AHUSHISHWA



IKIWA ni siku chache tangu Ofisa madini wa  Mkoa wa Geita Eng Pius R. Lobe kuwaamuru wavamizi waliaovamia eneo la Nyantorotoro kuondoka mara moja  na kumpisha mwekezaji mwenye leseni Majaliwa Maziku kufanya shuguli zake.

Kumezuka utata  baada ya M/Kiti wa CCM Mkoa wa Geita  Joseph  Msukuma kutajwa kuhamasisha wananchi kuvamia eneo hilo tena kwa ajili ya kufanya fujo.

Jambo hilo la kushangaza na kusikitisha limetokea jana majira ya saa tano asubuhi ambapo M/Kiti alikwenda katika eneo hilo  na  wananchi wa kijiji hicho na kuanza kufanya fujo huku wakilazimishwa kuingia ndani ya eneo hilo wakidai hawajalipwa sitaiki zao.

Wafanyakazi wa mwekezaji waliokutwa wakiendelea na kazi katika eneo hilo waliamua kutimua mbio mara baada ya wananchi hao kuingia kwenye eneo hilo na kuendelea kuponda kokoto mpaka watakapolipwa sitaiki zao.

“Jamani mimi kama M/Kiti wa CCM nasema msiondoke katika eneo hili endelea kuponda kokoto mpaka mlipwe haki zenu zote na hakuna wa kuwafukuza hata awe nani” alisema Msukuma.

Baada ya muda mfupi jeshi la polisi likiongozwa na OCD wa Wilaya ya Silvester Ibrahim Geita walifika na kuamuru wavamizi hao kuondoka mara moja kwa hiyari yao na walikubali kuondoka wao pamoja na M/Kiti huyo.

Afisa Madini wa Mkoa wa Geita  Eng. Pius R. Lobe alisema kuwa wao wanafuata sheria inasema nini na si wanasiasa na huyo M/Kiti anawanganya na atawaingiza matatani kwani watakamatwa na kufikishwa mahakamani bila kujali nani wala nani. Na kuongeza kuwa hakuna mtu yoyote anayedai, watu wate walishalipwa zamani na kutafutiwa eneo jingine.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita Omary Manzie Mangochie aliwataka wananchi wa eneo hilo kuacha kusikiliza siasa za kiongozi huyo bali wafuate sheria za nchi wasije wakaumia bure  na kuacha familia zao zikihangaika.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: