Kuanzia mwishoni mwa wiki iliyopita kulikua na stori
imesambaa sana kwenye mitandao ya kijamii kama instagram, facebook na twitter
kuhusu msichana wa kazi ambae alitegeshewa na Baba mwenye nyumba kamera
nyumbani na baadae video iliyorekodiwa ikamuonyesha akimpiga mtoto wa mwenye
nyumba.
Msichana
huyu wa kazi anaitwa Tumuhairwe ana umri wa miaka 22 na sio 25 kama
ilivyoripotiwa ambapo ana siku 26 tu toka aanze kufanya kazi kwenye familia ya
mtoto huyo.

Kwa sasa yuko rumande kwenye gereza
la Luzira Uganda na atafunguliwa mada ya kutaka kuua.
– Unaambiwa haya yote yasingejulikana kama Polisi isingemkamata baba mzazi wa mtoto huyu, yani baba alipoona ile video ndio akampiga Msichana huyu wa kazi ambae baada ya kipigo alikwenda kumshitaki baba wa mtoto Polisi.
Polisi walipomchukua Erick Kamanzi
(Baba wa mtoto) nyumbani kwa ke na kumfikisha Polisi ambako alieleza sababu za
kumpiga Msichana huyu na kuwaonyesha Polisi hii video hapa chini ambayo ni ya
tukio la mtoto wake kupigwa.
Baada ya hapo Polisi ndio
wakamwachia na kumkamata Msichana huyu wa kazi.
Erick ambae ndio baba mzazi wa mtoto
huyu amesema wanashukuru Mungu mtoto kuwa hai bila matatizo na sasa mtoto
amekua karibu na baba yake zaidi.
Tarehe 8 December ndio atapandishwa
Mahakamani kusomewa mashitaka yake.
November 24 2014 Waziri wa mambo ya
vijana wa Uganda aliitembelea familia ya mtoto huyu baada ya watu kuanza
kusambaza habari kwamba mtoto huyu alifariki, taarifa ambazo sio za kweli.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment