MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 16 December 2014

ALIVYOKUFA MGOMBEA UENYEKITI CCM MWANZA, TAZAMA HAPA



Mgombea Uenyekiti kupitia Chama cha CCM Mtaa wa Swea kata ya Mkolani Mwanza Pius Mihayo amefariki dunia gafla akiwa mtaani kwake muda mfupi baada ya kupiga kura.

Msimamizi wa uchaguzi huo Halifa Hida alisema mgombea huyo alifariki dunia gafla akiwa kwenye mtaa wake wa Swea na chanzo cha kifo chake hakijajulikana.

“Sasa kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi,tutatangaza matokeo ya wajumbe na nafasi za wagombea wa vitimaalum,nafasi ya uenyekiti haitatangazwa hadi taratibu nyingine za uchaguzi zitakapoandaliwa”alisema Hida.

Mkoani Arushamsongamano wa wapigakura katika kituo chaMbauda kata ya Sombetini unadaiwa kusababisha kifo cha mtu aliyetambulika kwa jina la Suleiman Bakari.

Tukio hilo lilitokea saa 3 asubuhi katika kituo hicho ambacho kilikua kimefurika watu ambapomtu huyo alianguka gafla baadaya kukosa hewa akiwa kwenye mstari wa kupigakura.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: